Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Water and Irrigation Wizara ya Maji 556 2023-06-07

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza:-

Je, lini Serikali italeta mradi wa kuhifadhi Mazingira katika chanzo cha maji cha Mto Ruaha na shamba la miti la Sao Hill?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inatambua umuhimu wa kuhifadhi mazingira na kulinda vyanzo vya maji kwenye maeneo mbalimbali nchini ikiwemo chanzo cha Mto Little Ruaha kilichopo kwenye Shamba la Miti la Sao Hill. Mto huo ni chanzo cha maji kwa wananchi wa Mji wa Iringa na viunga vyake na unatumika kwa shughuli za uzalishaji umeme, ufugaji na kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jitihada mbalimbali za kutunza vyanzo hivyo zinaendelea ikiwemo kuanzisha Jumuiya nne za Watumia Maji Wilaya za Mufindi, Kilolo na Iringa; kutoa elimu ya uhifadhi wa vyanzo; na kutekeleza program ya kupanda miti rafiki na maji ambapo miti 3,000 imepandwa katika halmashauri hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara inaandaa Mpango wa Uhifadhi wa Vidakio wa mwaka 2021 hadi 2035. Kwa kupitia mpango huo, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024, Serikali imepanga kuweka alama ya mipaka ya kudumu katika chanzo cha Mto Little Ruaha ndani ya Shamba la Miti la Sao Hill; kuweka mabango yenye jumbe za katazo za shughuli za binadamu katika chanzo cha uhifadhi wa chanzo; kupanda miti rafiki na maji; kutoa elimu kuhusu umuhimu wa uhifadhi endelevu wa vyanzo vya maji na mazingira; na kuajiri walinzi wa kulinda vyanzo vya maji kwenye shamba hilo hususani kwenye maeneo yenye uharibifu.