Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa Kata ya Tambukareli na Jeshi la Wananchi wa Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza nishukuru Serikali kupitia Jeshi la Wananchi Tanzania kwa malipo ambayo wameshayafanya katika Kata ya Mbugani huko Usule ambako wananchi wote waliokuwa wanahusika wameshapewa malipo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu lilikuwa, huko kwenye buffer zone ambako ni Tambukareli; je, jeshi wana mpango gani wa kuhakikisha wanaonesha kabisa kwamba haya ni maeneo yao na haya ni maeneo ya wananchi ili kuondoa huu mgogoro uliopo? Wao hawana tatizo na eneo la jeshi, tatizo lao ni kujua mipaka ya jeshi iko wapi na wao wanaishia wapi? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimepokea pongezi kutoka kwa Mheshimiwa Hawa Mwaifunga kwa Jeshi la Wananchi Tanzania na ninaomba kujibu swali lake kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya Bunge hili nimuahidi Mheshimiwa Mbunge nitaambatana naye ili tufike eneo hili pamoja na Idara ya Miliki na Majenzi kutoka Wizarani ili tuweze kuangalia changamoto hii, lakini niwahakikishie wananchi wa maeneo haya tutaweka mipaka bayana ili wananchi wajue wanaishia wapi na jeshi linaishia wapi, ahsante sana. (Makofi)