Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 555 2023-06-07

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa Kata ya Tambukareli na Jeshi la Wananchi wa Tanzania?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo linalozungumziwa lipo katika Kambi ya Jeshi Usule katika Manispaa ya Tabora. Eneo hilo la Jeshi lilipimwa na ramani yake kusajiliwa Mwezi Septemba, 2004 na kupewa nambari 41,574. Mwezi Februari, 2023 Wizara imepeleka fedha kiasi cha shilingi 194,029,643 kwa Manispaa ya Tabora kwa ajili ya kugharamia fidia kwa wananchi wa maeneo ya Usule na Itaga waliopo katika eneo la Jeshi na tayari wahusika wameshalipwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua zipo changamoto za mipaka katika eneo la buffer zone katika Kata ya Tambukareli. Naelekeza Idara ya Miliki na Ushauri Majenzi katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kufika eneo hili na kuainisha changamoto hizi na kuzipatia ufumbuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inaendelea kusisitiza wananchi kutovamia maeneo ya Jeshi, kwani ni hatari kwao na mali zao, ahsante sana. (Makofi)