Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza:- Je, ubunifu una nafasi gani katika kuleta mageuzi ya kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kuna ongezeko kubwa la thamani ya bidhaa zinazotokana na ubunifu, kwa mfano, kutoka mwaka 2002 kulikuwa na shilingi bilioni 208, kufikia mwaka 2020 zaidi ya shilingi bilioni 700 kwa takwimu za Umoja wa Mataifa. Je, Serikali imejipangaje kulinda hakimiliki za wabunifu wa Kitanzania ili washiriki kikamilifu katika uchumi bunifu wa dunia?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa uchumi bunifu na bidhaa bunifu ni utajiri wa kibiashara na kiutamaduni. Je, Serikali haioni wakati umefika sasa Wizara ya Elimu kushirikiana na Wizara ya Utamaduni, Wizara ya Fedha na taasisi nyingine za kibiashara kuona kwamba Tanzania inashiriki kikamilifu katika uchumi bunifu katika dunia yetu? Nashukuru.

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Londo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inajitahidi kwanza kuchochea bunifu mbalimbali hapa nchini na kuanzia mwaka 2019, Serikali imekuwa ikiendesha Mashindano ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu maarufu kama KISATU kwa ajili ya kualika watu mbalimbali walete bunifu zao, washindanishwe, zitambuliwe na ziendelezwe. Baada ya kuendelezwa ziweze kulindwa kwa kupata hakimiliki. Tangu tuanze mashindano hayo tayari bunifu 283 zimeshahakikiwa, 38 tayari ziko sokoni nazo hizo zinalindwa kwa ajili ya kuingia sokoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla wake Serikali inaona umuhimu sana wa kuchochea bunifu kwa ajili ya maendeleo ya uchumi, ndiyo maana vile vile tunasaidia vijana wetu ambao wanaenda na bunifu mbalimbali katika mashindano ya Kimataifa na baadhi yao wameshinda tuzo mbalimbali na sisi tunachochea waingie sokoni kwa ajili ya kubiasharisha bunifu zao.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza:- Je, ubunifu una nafasi gani katika kuleta mageuzi ya kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Je, Serikali ina mpango gani wa kutambua na kuendeleza ubunifu unaofanywa na wanafunzi kwenye vyuo vyetu hapa Tanzania kikiwepo Chuo cha DIT ambapo kuna mwanafunzi mmoja anaitwa Angella Cliff Nkya ametengeneza mfumo wa ku-control makosa ya barabarani ili waweze kuendelezwa na Serikali?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua bunifu zote za wanafunzi na watu mbalimbali hata watu walioko vijijini na wanafunzi wamechangia vile vile katika baadhi ya bunifu ambazo sasa hivi zimeanza kuingia sokoni. Zipo bunifu ambazo tayari zimeshaanza kutambulika, zinafahamika na hatua iliyobaki kwa kweli sasa hivi ni kuhakikisha kwamba bunifu hizo zinaingia sokoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nitoe mfano mmoja tu, bunifu ya kuweza kulipia bili ya maji kwa kutumia simu janja ambayo imegunduliwa na Mtanzania, sasa hivi inafanyiwa majaribio kwa ajili ya kununuliwa na Mamlaka ya Maji Tanzania na kutumika.