Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 553 2023-06-07

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza:-

Je, ubunifu una nafasi gani katika kuleta mageuzi ya kiuchumi?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ameir Abdalla Ameir, Mbunge Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ubunifu ni nyenzo na kichocheo cha kuongeza ufanisi katika sekta mbalimbali za uzalishaji na kutoa huduma nchini. Matumizi ya ubunifu yameongeza ufanisi katika uzalishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma. Aidha, maeneo yaliyonufaika zaidi ni pamoja na: mawasiliano, huduma za fedha, utawala, masoko, afya, tafiti na usimamizi wa fedha za umma, mitambo inayojiendesha, kompyuta na roboti.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ubunifu wa teknolojia mpya ikiwemo mifumo ya TEHAMA katika undeshaji wa shughuli za Serikali (e-Government) na kukusanya mapato ya serikali kwa njia ya kielektroniki (GePG) kwa kiasi kikubwa zimechangia katika mageuzi ya kiuchumi tunayoshuhudia nchini. Mathalan ubunifu uliowezesha kutuma na kupokea fedha kupitia simu za mkononi, umeleta mageuzi makubwa ya kiuchumi nchini hasa kwa wafanyabiashara na wananchi mijini na vijijini.