Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka utaratibu mzuri wa kutambua fire hydrants nchini na kuziwekea alama ili kusaidia wakati wa majanga ya moto?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini na maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa fire hydrants zinazotakiwa nchini ni 285,000 na zilizopo ni 2,348 sawa na asilimia 8.2 tu;

Je, Serikali haioni haja ya kujenga miundombinu hiyo ili kuzuia majanga makubwa ya moto yanatokea ili kuzuia pia Serikali kupata hasara na wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa changamoto hii inatokea katika miji na majiji makubwa;

Je, Serikali haiona sasa kuna haja ya kuweka miundombinu hiyo katika miji na majiji makubwa, kwenye masoko na shule ili pia kuzuia majanga hayo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, ninakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba fire hydrants zilizopo ni chache hazilingani na zile zinazohitajika, na ndiyo maana Jeshi letu la Zimamoto na Uokozi linawasiliana na mamlaka zote za ujenzi za miji pamoja na mamlaka za maji kila wanapotekeleza miradi hiyo wazingatie uwekeji wa hizi fire hydrants.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili ninakubaliana naye, kwamba miji mikubwa ndiyo iko kwenye changamoto kubwa zaidi ya kukumbana na majanga ya moto na kwa msingi huo mkazo zaidi utawekezwa kwenye miji mikubwa kadiri tunavyoendelea kuimarisha huduma za fire na uokozi.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka utaratibu mzuri wa kutambua fire hydrants nchini na kuziwekea alama ili kusaidia wakati wa majanga ya moto?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, aah! Sorry, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Je, Serikali imewaandaje Askari wa Jeshi la Zimamoto katika uokoaji kwenye uvamizi wa nyuki katika makazi ya watu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kama ambavyo jukumu lake limebainishwa linashirikiana na mamlaka za misitu kila inapotokea janga kama hilo la nyuki kama ilivyotea siku tatu zilizopita hapa Dodoma, wameshirikiana vizuri sana wenzetu wa idara ya misitu kukabiliana na janga lile na kuwahamisha kabisa nyuki kutoka eneo lile. Nadhani ni jambo ambalo tunaomba wananchi inapotokea makundi ya nyuki kwenye maeneo yao wapige namba ya dharura inayoonyesha always 114 ili vyombo vyetu viweze kukabiliana nayo kabla haijaleta madhara kwa jamii zetu, nashukuru.