Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 551 2023-06-07

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: -

Je, lini Serikali itaweka utaratibu mzuri wa kutambua fire hydrants nchini na kuziwekea alama ili kusaidia wakati wa majanga ya moto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeshirikiana na Mamlaka za Miji na Maji kukagua na kutambua fire hydrants 2,348 ambazo zipo Nchi nzima. Jeshi limeanza kutekeleza utaratibu maalum wa kimataifa wa utambuzi wa fire hydrants ambao ni kuziwekea alama ya FH. Jeshi pia linaziweka fire hydrants hizo katika mfumo wa utambuzi Kijiografia (Geographical Information System – GIS) na kuzijengea mifuniko migumu itakayozuia uharibifu wake. Aidha, Jeshi linawasiliana na mamlaka zinazohusika na ujenzi wa barabara na uendelezaji wa miji kudhibiti ujenzi holela wa makazi na upanuzi wa barabara za mitaa unaohusisha kuzifukia fire hydrants. Lengo ni kuzitunza fire hydrants zilizopo ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji wakati wa kutelekeza majukumu ya kuzima moto yanapotokea majanga, nakushukuru.