Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza:- Je, nini kauli ya Serikali kuhusu ucheleweshaji fedha zinazotumwa Nje ya Nchi kutokana na Mabenki kuwa na uhaba wa fedha za Kigeni?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Niishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa mabenki mengi hapa nchini bado yana uhaba wa fedha tofauti na Mheshimiwa Waziri ulivyosema. Hali ambayo imepelekea sasa hivi wafanyabiashara wengi wa Soko la Kariakoo, hawa wadogo wadogo na wengine wakubwa wanapata shida ya kupata pesa za kigeni, kiasi kwamba CRDB in a day sasa hivi huwezi kupata zaidi ya dola 1,000 na mabenki mengine kama NMB na NBC huwezi kutoa zaidi ya dola 500 kwa siku. Kitu ambacho kama mtu anahitaji kutuma pesa nyingi nje ina mchukua muda mrefu sana kuzunguka kwenye benki mbalimbali kukusanya hela na haruhusiwi ku-change hizo hela;

Je, sasa ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha tunawapeleka wafanyabiashara katika dreams zao za kupata fedha za kigeni ili waweze kufanya shughuli zao za biashara vizuri bila kukwama? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kihalisia Nchi zetu zimekuwa zinafanya trading kubwa sana na Nchi za Asia ikiwemo China, India na Uturuki pia, lakini wafanyabiashara wa Tanzania wanalazimika kubadilisha pesa zao kuwa kwenye shilingi kupeleka katika dola na wanapofika kwenye yale Mataifa wana-change tena kutoka kwenye dola kupeleka kwenye pesa za wale mataifa;

Je, sasa wanakuwa wanapata hasara ya exchange rate hapo, hamuoni kwamba iko hajia ya Serikali ya Tanzania kuongea na mataifa haya makubwa ambayo tunafanya nayo biashara na tunatembelea kwa kiasi kikubwa na uanguko wa dola hasa zinaposhindwa kupatikana, wakaturuhusu tukaanza kufanya exchange rate ya pesa za nchi zao; kwa mfano anaenda China akaondoka na Yuan akiwa hapa hapa akifika kule asipate usumbufu wa kubadilisha kwenye dola halafu watoke kwenye dola warudi kwenye pesa ya Mataifa yao?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Chiwelesa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi, tayari Serikali imechukua hatua kadhaa ili kupunguza au kuondoa changamoto hiyo. Kwa hiyo naomba nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, hivi karibuni changamoto hiyo imeondoka katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, shauri lako Mheshimiwa Engineer tumelichukua na tunalifanyia kazi. Ninachotaka kukuambia, hivi karibuni tumeanza mazungumzo na India katika shauri ambalo umelitoa na Nchi nyingine tutaenda.