Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE K.n.y. MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, lini Benki ya CRDB itafungua tawi katika Mji wa Mangaka?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mwezi Septemba ni mwezi ambao tunategemea kuanza kilimo katika maeneo yetu;

Je, Serikali haioni haja ya kuwataka Benki ya CRDB waanze kutoa mikopo kwa wakulima ili waweze kutayarisha mashamba yao? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Kata za Msikisi, Kijiji cha Namalembo na Matutwe, Chiwalwe, Namajani pamoja na Mpanyani zipo mbali sana na makao makuu ya wilaya ambako ndiko zinatolewa huduma za kibenki kwenye Jimbo la Ndanda;

Je, Serikali haioni haja ya kuwasogezea wananchi huduma kwenye maeneo hayo?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu Maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwambe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba benki itatoa huduma zote mara tu baada ya kukamilika kule Liwale ikiwemo mikopo CSR na mengineyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, tutashauriana na benki ili wapeleke huduma hizo za kibenki katika zile kata ambazo hazijafikiwa na benki ili kuepusha utapeli ambao unafanyika katika shughuli za wanadamu kiuchumi za kila siku.