Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Mnyamasi ili Barabara ya Kambanga-Ifinsi hadi Bungwe iweze kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa kufanya jitihada za kupeleka mradi hasa wa ujenzi wa Daraja la Mto Mnyamansi. Kwa kuwa eneo la Ifinsi kwenda Kijiji cha Bugwe hakuna mawasiliano ya aina yoyote. Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hiyo ili iweze kuwasaidia wananchi kwenye eneo hilo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili tunatambua jitihada za Serikali zilizofanywa, mmefungua barabara ya Kamibanga hadi Ifinsi, Majalila hadi Ifinsi lakini barabara zote hizo zilizofunguliwa hazijawekewa molamu na madaraja. Ni lini Serikali itaanza kujenga na kuboresha barabara hizo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kakoso. La kwanza juu ya mpango wa ujenzi wa barabara hii ya Ifinsi – Bugwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba barabara hii haikuwepo na ilikuwa wananchi hawa wanakaa kwenye kisiwa kipindi ambapo mvua zinanyesha. Tayari baada ya utengaji huu wa bajeti ya 1.5 billioni, Serikali pia katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 imetenga kiasi cha shilingi milioni 475 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha changarawe kwenye vipande korofi na kuweka mifereji katika maeneo mbalimbali ya barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili lla Barabara za Kambanga – Ifinsi na maeneo mengine aliyoyataja Mheshimiwa Kakoso tutakaa naye Mheshimiwa Mbunge na kuona ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ukarabati na kuweka kifusi katika barabara hizi.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Mnyamasi ili Barabara ya Kambanga-Ifinsi hadi Bungwe iweze kutumika?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mwamkulu – Kakese hadi Misunkumilo yenye kilometa 30 kwa kiwango cha lami kupitia TACTIC Awamu ya Pili?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Mwakulu – Kakese ipo katika mpango wa ujenzi wa mradi ule wa TACTIC na hivi karibuni watatangaza kazi ya kuweza kuwapata wale watakaofanya usanifu wa barabara hii na itaanza ujenzi wake kwa vipande. Kwa hiyo, wakipata wale watu wa kwenda kufanya usanifu tutamjulisha Mheshimiwa Kapufi ili naye aweze kushiriki katika zoezi la utiaji saini kama ambavyo tulifanya kwenye miradi mingine ambayo ipo chini ya TAMISEMI.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Mnyamasi ili Barabara ya Kambanga-Ifinsi hadi Bungwe iweze kutumika?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa. Je, ni lini Serikali itajenga daraja la kutoka Mlambalasi ambayo ni Kata ya Kiwere kwenda Kalenga ambako ndiko kwenye Makumbusho ya Chifu na wananchi wamekuwa wakipata shida sana? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuweza kupitia bajeti ya TARURA ya mwaka 2023/2024 na kuona ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili la Mlambalasi kuelekea Kalenga; na kama bajeti imetengwa tutahakikisha mara moja fedha hiyo inakwenda ili ujenzi huu uweze kuanza.