Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 548 2023-06-07

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Mnyamasi ili Barabara ya Kambanga-Ifinsi hadi Bungwe iweze kutumika?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto wanayopata Wananchi wa Kijiji cha Kambanga-Ifinsi wakati wa kuvuka Mto Mnyamasi na inaendelea kufanya jitihada mbalimbali kukabiliana na changamoto hiyo. Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Serikali kupitia TARURA imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo. Mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 11 Mei, 2023 na Mkandarasi yupo kwenye hatua ya maandalizi ya kuanza kazi ambayo inatarajiwa kukamilika Februari, 2024.