Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kupata viwanja vya michezo na kuvilinda kwani baadhi ya shule zimetumia kujenga madarasa?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Kwa kuwa club nyingi ambazo zinaanzishwa hapa nchini zimekuwa zikitumia maeneo ya taasisi ambayo sasa hivi ni machache na sehemu zingine hakuna kabisa. Ni upi mkakati wa Serikali wa Kitaifa wa kuhakikisha kwamba tunakuwa na maeneo ya public ambayo ni theme ya michezo mbalimbali nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili hivi karibuni Serikali ilitangaza ajira za walimu takribani 15,000. Nataka kufahamu katika idadi hiyo ya walimu ni walimu wangapi wenye taaluma ya michezo ambao wamechukuliwa kwa taaluma yao na kupelekwa kwenye halmashauri kama ajira ya Serikali? Nakushuru sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kanyasu la kwanza nini mkakati wa Serikali kuwa na maeneo yake ya michezo na kuacha kutegemea taasisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni tumeona mbele ya Bunge lako hili Wizara ya Michezo ikipitisha bajeti yake na tayari kwa mfano hapa Dodoma wana mkakati wa kujenga uwanja pale katika eneo la nane nane ambalo litakuwa linamilikiwa na Serikali. Katika mikoa mingine vivyo hivyo wameendelea kuweka mpango kwa ajili ya kuwa na maeneo ya wazi na tutashirkiana na wenzetu wa Wizara ya Michezo kuona ni namna gani tunaweka kipaumbele hicho katika kujenga maeneo haya ili wanafunzi waweze kufanyia mazoezi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili kwenye idadi ya walimu walioajiriwa hawa hivi karibuni ni wangapi ni walimu wa michezo. Nitakaa na Mheshimiwa Kanyasu ili kuona katika orodha hii ya majina ambayo hivi karibuni Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ametangaza ni walimu wangapi ambao wameingia wa kada ya michezo.