Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 547 2023-06-07

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kupata viwanja vya michezo na kuvilinda kwani baadhi ya shule zimetumia kujenga madarasa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Costantine John Kanyasu, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mojawapo ya vigezo vya kuanzishwa shule ni pamoja na uwepo wa viwanja vya michezo. Michezo ni muhimu kwa kuwa husaidia kuimarisha afya za wanafunzi na kujenga akili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) itafuatilia jambo hili na kujiridhisha, endapo kuna shule ambayo imetumia viwanja vya michezo kujenga madarasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa rai kwa Walimu Wakuu, Wakuu wa Shule pamoja na Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuzingatia kanuni na taratibu zote zinazohusu usajili na uendeshaji wa shule ikiwa ni pamoja na kulinda miundombinu iliyopo shuleni kama viwanja vya michezo.