Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamagome?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwenye swali langu la msingi. swali la kwanza ni lini sasa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na hao wataalam wa TAMISEMI uliowasema watafanya tathmini hiyo ya kujenga kituo cha afya pale Kwamagome?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ahadi hii ya ujenzi wa kituo cha afya ilifanywa kwenye mkutano wa hadhara na Waziri wa TAMISEMI.

Je, uko tayari baada ya Bunge hili la bajeti tuambatane mpaka Kata ya Kwamagome ili ukawaeleze wananchi kwa nini ahadi hii haijatekelezwa kwa miaka miwili tangu imetolewa? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kwagilwa hili la kwanza la Ofisi ya Mganga Mkuu lini itaenda na hii timu ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Naomba nitumie Bunge lako hili Tukufu kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga pamoja na timu yetu ya tathmini iliyopo Ofisi ya Rais TAMISEMI kuhakikisha wanafika katika Halmashauri ya Mji Handeni na Kata ya Kwamagome kwa ajili ya kufanya tathmini na kuona kama idadi ya watu inayohitajika na ukubwa wa kata ile vinakidhi vigezo vya kupata kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili naomba nisisitize wafanye hivyo mara moja huku wakiwasiliana vilevile na Mheshimiwa Kwagilwa ili aweze kuwepo kwa niaba ya wananchi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pii nipo tayari kuongozana na Mheshimiwa Kwagilwa kuweza kufika Kata ya Kwamagome.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamagome?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Kemgesi pamoja na Ligicha Wilayani Serengeti?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ni majuzi tu ambapo tulikaa na Mheshimiwa Mrimi aliwasilisha maombi haya katika Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya kituo cha afya Kemgesi na kadiri ya upatikanaji wa fedha tutahakikisha Mheshimiwa Mrimi kule wanaserengeti wanapata kituo hichi cha afya.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamagome?

Supplementary Question 3

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, je, lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye Kata za Bwawani, Bangata, Kidina, Otoroto na Kimnya kwenye Jimbo la Arumeru Magharibi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu kuweza kuona kwenye bajeti ya mwaka 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya hivi ndani ya jimbo lake na pale ambapo fedha imetengwa tutahakikisha inaenda mara moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo hivi vya kata.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamagome?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Sangamwalugesha Wilaya ya Maswa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaanza ujenzi wa vituo hivi vya afya ambavyo amevitaja Mheshimiwa Mbunge Wilayani Maswa kadiri ya upatikanaji wa fedha.