Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 546 2023-06-07

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamagome?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha wa 2020/2021, Halmashauri ya Mji Handeni, ilitengewa shilingi milioni 50 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa zahanati ya Kwamagome na mwaka wa fedha wa 2021/2022 shilingi milioni 50 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati ya Kwaluwala katika Kata ya Kwamagome.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshatoa jumla ya Bilioni 117 kwa ajili ya kuimarisha huduma za afya ya Msingi kwa ujenzi wa vituo vya afya kwenye Kata za kimkakati kote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga pamoja na wataalam wa Ofisi ya Rais (TAMISEMI), watafanya tathmini ya kina kuhusu kata hii na mara fedha zitakapopatika Kituo cha Afya katika Kata ya Kwamagome kitajengwa.