Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara za vijijini zinazopita katika vilima vikali?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali kwanza tunaishukuru lakini nataka kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ili barabara hii ilete ile tija ambayo imekusudiwa ni vyema ikakamilika kwa haraka ili kunusuru maisha ya wananchi pamoja na mali zao. Ni upi sasa mkakati wa Serikali wa kuhakikisha barabara hii inatengewa fedha za dharura ili iweze kukamilisha ujenzi kwa haraka iwezekanavyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, jiografia ya Wilaya ya Newala kila upande ambao utaingilia unakutana na vilima vikali. Kwa mfano Nadimba Chiwata, Mikumbi, Mpanyani, Mkoma II Chimemena, Lihanga Chikalole. Ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba barabara hizi ambazo nimezitaja zinajengwa angalau kwa kiwango cha changarawe? nakushukuru.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mtanda la kwanza la mpango wa dharura.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimekwishakusema katika majibu yangu ya msingi kwamba Serikali katika mwaka wa fedha huu ambao tupo sasa tumeutekeleza ilitenga shilingi milioni 825 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii. Mwaka wa fedha tunaoenda kuuanza mwezi Julai 2023/2024 TARURA imetenga shilingi bilioni moja na tayari bado matengenezo haya yanaendelea na yapo asilimia 52.

Mheshimiwa Naibu Spika, tutaendelea kuhakikisha kwamba hii bilioni moja inaenda haraka katika Jimbo la Newala Vijijini kwa ajili ya kutekeleza kipande cha barabara ambacho kimetengwa kwa utekelezaji wake ili wananchi waweze kupita kwa sababu barabara hii inaunganisha Jimbo la Ndanda na Jimbo la Newala Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Mwambe na Mheshimiwa Mtanda wamekuwa wakifatilia sana barabara hii. Nikienda kwenye swali lake la pili la barabara hii ambayo inapita Nandimba, Chiwata ambayo inatoka Newala Vijijini kuelekea Masasi tutaendelea kutafuta fedha na kutenga fedha kwa ajili ya kutengeneza barabara hii na kipaumbele kikiwa katika maeneo ya vilima vikali.