Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 544 2023-06-07

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara za vijijini zinazopita katika vilima vikali?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilitenga fedha shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa barabara kilometa mbili kwa kiwango cha lami katika Kilima Kikali wa Miyuyu - Ndanda na kazi imekamilika. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, shilingi milioni 825 zimetengwa kwa ajili ya kujenga kilomita mbili za lami, kilometa mbili kwa kiwango cha changarawe na kujenga daraja dogo (box culvert) moja katika kilima hicho ambapo kazi hizo zinaendelea kutekelezwa na zimefikia asilimia 52.2 ya utekelezaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 jumla ya shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara kilometa moja kwa kiwango cha lami katika kilima kikali cha Miyuyu-Ndanda na kiasi cha shilingi milioni 300 kimetengwa kujenga kilometa 0.5 kwa kiwango cha zege kwenye eneo la kilima katika Barabara ya Malatu Juu – Mnauke – Mitahu -Mkululu yenye urefu wa kilometa 16.4.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kufanya usanifu na kujenga barabara zenye changamoto ya vilima vikali kwa kiwango cha lami kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha kwa kila mwaka.