Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Mimi ni Mbunge wa Tarime Vijijini, pale Nyamwata, Kerende, Nyangoto ni vijijini kabisa. Maeneo haya yote wananchi wanalipa umeme kwa gharama kubwa. Kwa hiyo, Jimbo limegawanywa kuna watu wanalipia umeme kwa bei ya chini ya shilingi 27,000 na wengine bei kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nijue ni lini mchakato huu wa kurudisha bei ya shilingi 27,000 ya umeme kwa watu wa vijijini inarudishwa ili watu wapate umeme sawa? Huu mchahakto umechukua muda mrefu.(Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwikwabe Waitara, kwamba ni kweli tumebaini yapo maeneo mengi ambapo tulipofanya tathmini awali tumeyaacha, wale wataalam wameelekezwa warudi tena ili wakifanya iwe ni once and for all. Kwa hiyo, wanapita kwenye maeneo yetu, kazi ni kubwa inahitaji weledi na utulivu mkubwa ili tuweze kuwahudumia wananchi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Waitara na Waheshimiwa Wabunge mtuvumilie kidogo tulikamilihse hili kwa usahihi na ufasaha kabisa. Tutakapokuja kuleta mbele yenu liwe ni tatizo ambalo tumelikamilishwa tuende kwenye hatua nyingine. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na sintofahamu sana kwa wananchi wengi wakiwepo wa Jimbo la Kibamba kubambikiwa madeni makubwa ya ununuzi wa umeme au LUKU bila kuelewa kutokana na kukosewa kwa makadirio ya awali na TRA. Je, Serikali mko tayari kuwaelekeza TRA waweke mpango mzuri ambao wananchi hawa wataweza kupunguza madeni yale kila mwezi wakiwa wanalipa LUKU zao kila mwezi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Mtemvu, kwa swali lake. Juzi wakati tunapitisha bajeti jambo hili lilijitokeza na ulitolewa Mwongozo na Mheshimiwa Spika kwamba, Wizara ya Nishati pamoja na wenzetu TRA ambao hasa ndiyo wenye hizo pesa tukae na kuweka utaratibu mzuri. Sisi tumeshawafikishia wenzetu, tumewapelekea concern hiyo wanatengeza utaratibu mzuri wa kuonesha deni na mwananchi aweze kulipa taratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hili Wizara ya Nishati kupitia TANESCO ni kama bomba la kupitisha mapato hayo ambayo yanatoka kwa mwananchi kupitia TRA. Hata hivyo, tunashirikiana na wenzetu kuweka mifumo mizuri ili wananchi wanaopata huduma ya umeme sasa wasipate adha ya kulipa kodi hii ya majengo ambayo inapitia kwetu. Kwa hiyo, tutalifanyia kazi kwa pamoja Serikalini.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ambayo Wizara hii ndiyo Wizara pekee iliyotengewa bajeti ya zaidi ya shilingi trilioni tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa majibu ya Serikali ni mazuri vipo baadhi ya Vijiji – Miji vinavyofanana na hivi alivyovitaja ikiwemo Ibumila na maeneo mengine. Je, Serikali iko tayari sasa kuwapatia wananchi umeme kwa bei ya vijiji kama alivyotaja vikiwepo Vikwete, Mkolango na Malombwe?

Swali la pili, kwa kuwa wananchi wa Makambako wa Kata ya Kivavi na Kata ya Majengo wameathirika kwa muda mrefu wakisubiri umeme wa upepe na kulipwa fidia zaidi ya miaka 20. Je, Serikali inawapa majibu gani wananchi hawa ili kama haiwezekani wananchi waendelee na shughuli zao? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la kwanza la swali la Mheshimiwa Sanga, Serikali inayo nia ya dhati kabisa kuhakikisha kwamba wananchi wanaunganishiwa umeme kwa gharama nafuu ambazo wanazimudu. Kama tulivyosema juzi kwenye bajeti yetu, tunaendelea kufanya tathmini na upembuzi yakinifu kubaini ni maeneo gani yanaweza yakawa yanakidhi gharama hizo za shilingi 27,000 pia kutafuta chanzo kizuri na cha uhakika cha kuweka ruzuku katika eneo hilo, kwa sababu ni kweli gharama za kuunganisha umeme ni kubwa. Pale ambapo tunatakiwa kuunganisha kwa shilingi 27,000 basi inabidi kuwekwa ruzuku kubwa na tunapounganisha kwa 320,000 basi tunaweka ruzuku kama nusu. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Sanga na wengine wote kwamba jambo hili Serikali imeshalichukua na inalifanyia kazi tunaamini litakamilika siku chache zijazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la pili, ni kweli kwamba wananchi wa maeneo ya Makambako wameahidiwa kupewa umeme wa kutumia upepo na maeneo yao yalainishwa kwamba yatalipiwa fidia kwa muda mrefu. Tumechukua muda mrefu kwenye mazungumzo na wale waliotaka kuwekeza ninapenda kusema kwamba tumefikia hatua ya mwisho ya mazungumzo hayo, ambapo TANESCO tayari wamekwishatengeneza mkataba wa makubaliano na wanaupitisha kwenye taasisi yao na baadae utakuja Wizarani ili utolewe sasa kwa ajili ya kuendelea na hatua nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Makambako kabla ya mwezi wa Tisa shughuli zitaanza site kwa kulipa fidia na kuanza kutekeleza mradi utakaotuongezea umeme wa upepo kwenye gridi yetu ya Taifa.(Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Liwale unaoundwa na Kata tatu, Kata ya Likongole, Liwale Mjini na Nangando vipo vijiji zaidi ya kumi lakini vijiji vile vimegawanya, kuna vijiji vinalipa shilingi 27000 na kuna vinavyotakiwa kulipa shilingi 350,000. Je, Serikali haioni kwamba kwa sababu vyote hivi ni vijiji viingizwe kwenye kulipa shilingi 27000 ili kuweka usawa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nifafanue kidogo jibu ni lilelile lakini niliongezee nyama kidogo.

Mheshimiwa wenyekiti, Wizara ya Nishati kupitia TANESCO tulibaini maeneo ya Vijiji na Miji kutoka kwenye taarifa za wenzetu wa TAMISEMI ndiyo waliotupatia taarifa za hapa ni mjini na hapa ni kijijini. Baada ya ku– implement hicho tulichokipata ndiyo yakatokea maoni mbalimbali kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge na wananchi. Tukaona ni vema tuende site wenyewe ili tukabaini, pamoja na kwamba enzetu wa TAMISEMI wamesema hapa ni mjini lakini maisha ya pale yanaonesha kuwa ni kijijini na hilo ndilo zoezi tunalolifanya na tukilikamilisha tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ili kuweka usawa kama ulivyoshauri Mheshimiwa Kuchauka ili wananchi waweze kulipa ile gharama ambayo wanaweza kuilipa kutokana na mapenzi na utashi mwema wa Serikali kuhakikisha kwamba inawahudumia wananchi wake salama.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mimi nina swali moja.

Je, Serikali hamuoni umuhimu wa kumaliza utengenezaji wa umeme katika Jimbo la Temeke hasa Jimbo la Mjini, ukizingatia kuna wakati umeme unakatika kwenye viwanja hasa katika mechi hizi za Kimataifa, ni lini sasa mtarekebisha umeme huo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la Mheshimiwa Dorothy Kilave ni la msingi kabisa. Tunayo nia ya dhati kama Serikali kumaliza tatizo la kukatika umeme Tanzania nzima. Tunashukuru kwamba juzi mmepitisha bajeti ya Wizara ya Nishati yenye fedha za kutosha kwa ajili ya kuhakikisha tunaondokana na tatizo hili. Tuwahakikishie litakwisha kupitia mradi wetu wa gridi imara tutaendelea kuimarisha maeneo mengi ambayo yana changamoto kubwa ya ukatikaji wa umeme ikiwemo Jimbo la Temeke. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwepo na kukatwa kwa kodi za majengo kwa wale ambao hawastahilin kukwatwa kwa mfano, wazee na zile nyumba za tembe. Sasa, ninataka kujua ni lini Serikali itafanya reconciliation ili iweze kuwarudishia gharama zote ambazo wamekatwa hawa ambao hawastahili kukatwa kodi hizi za majengo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotangulia kusema na kama tulivyosema kwenye budget speech ya juzi, wenzetu wa Wizara ya Fedha wameshalichukua nasi tulichowa-supply ni namba za LUKU kwa ajili ya wao kuwa-identified nani anastahili kulipa kiasi gani na kwa wakati gani na kwa utaratibu gani. Tunashirikiana nao wenzetu ili waweze kuweka utaratibu mzuri ambao utahakikisha yule anayetakiwa kulipa kweli ndiye anayelipa kama tulivyosema juzi kiwanja kimoja kinaweza kuwa kina vyumba vitano, sita halafu kila mmoja analipa wakati hakutakiwa kulipa kilo mmoja, lakini tunafahamu pia sheria nyingi zinaeleza kwamba wale wazee wa miaka 60 na zaidi wawe-exempted kwenye hayo maeneo na wastaafu wengine tumeshawasiliana na wenzetu na tunalifanyia kazi naamini wenzetu wa Wizara ya Fedha watakamilisha na tutafikia sehemu nzuri.