Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 524 2023-06-05

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapitia upya uhalisia wa malipo ya umeme kwa Vijiji vya Mkolango, Kiumba, Ikwete na Malombwe ambapo walilipia kwa bei ya Mjini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Vijiji vya Ikwete na Mkolango, wananchi wote wa maeneo hayo wanalipia gharama ya shilingi 27,000 kwa ajili ya kuunganishiwa umeme. Aidha, Vijiji vya Malombwe na Kihumba ni miongoni mwa vijiji vyenye sura ya Vijiji-Miji ambavyo kwa tathmini ya awali, vilionekana vinastahili kulipia shilinigi 320,960 kama garama ya kuunganishiwa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kubaini changamoto katika tathmini ya awali, Serikali kupitia TANESCO inaendelea kufanya tathmini ya maeneo yote yenye sura ya Vijiji-Miji yakiwemo maeneo ya Malombwe na Kiumba ili kuyapatia suluhisho la gharama za kuunganishiwa umeme. Serikali inaendelea kuomba wananchi wa maeneo hayo wawe na subira wakati suala hili linashughulikiwa.