Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza huduma za afya na dawa zinazotolewa na Bima katika zahanati na vituo vya afya?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Kwa kuwa, Serikali imeshaongeza vifaatiba na dawa kwa zaidi ya asilimia 100 kwenye Zahanati na Vituo vya afya. Ni lini sasa watatoa hadhi kwenye vituo hivyo ili viweze kutoa huduma zote za Bima ya Afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Serikali inatambua kwamba yapo maeneo ambayo bado huduma hizi hazijafika na amesema ipo mikakati ya Serikali kwa ajili ya kufikisha huduma hizo. Ningependa kujua sasa ni ipi mikakati hiyo ya Serikali ili kuhakikisha kwamba Watumishi kwa maana ya rasilimaliwatu wanaongezeka, vifaatiba pamoja na miundombinu inaimarika? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake ambalo ni strategic kwa ajili ya kuboresha huduma za afya. Swali lake la kwanza kwamba ni lini vituo hivyo vitapewa vibali vya kusajili? Mheshimiwa Mbunge ni kwamba vituo vyote, zahanati, vituo vya afya ambavyo vimesajiliwa ni kwamba Bima wanatakiwa wawaruhusu pia kutumia dawa hizi ambazo ziko kwenye mwongozo wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge kama kuna zahanati au kituo cha afya chochote ambacho hakijasajiliwa nawaagiza Bima ya Afya wapitie nchi nzima wahakikishe vituo vyote ambavyo vimetimiza hivi vigezo basi viwe vimesajiliwa na kutoa huduma hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kuhusu kufikiwa vituo vingine. Moja, tunajua mwaka huu vifaa vingi sana vimenunuliwa na viko njiani vinakuja, kwa hiyo, vitasambazwa kwenye vituo vyetu lakini kwenye bajeti ya mwaka huu tunakwena ku–cover hivyo vituo na ajira zitaendelea kufanyika kila mwaka unaokuja kuhakikisha tunawafikia wote.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza huduma za afya na dawa zinazotolewa na Bima katika zahanati na vituo vya afya?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa dawa ya kisukari kwa wagonjwa wa sukari imekuwa ni changamoto sna kwenye vituo hivi vya afya mpakla waende Wilayani. Je, Serikali sasa haioni umuhimu wa ku-review utaratibu huu ili kwenye level za Vituo vya Afya pia waweze kupata?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo ambalo lilikuwa linaleta malalamiko mengi hasa kwenye zahanati na vituo vya afya hasa kwa wazee wetu wagonjwa wa kisukari na presha ni eneo hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amesema. Ukiona hapa tumeongeza dawa kwa kiasi hiki ni moja wapo ya dawa hizi za sukari na presha kuhakikisha sasa hiyo shida iliyokuwepo huko nyuma haitatokea tena.