Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 523 2023-06-05

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza huduma za afya na dawa zinazotolewa na Bima katika zahanati na vituo vya afya?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kuongeza huduma za afya na dawa zinazotolewa na bima katika Zahanati na Vituo vya Afya imefanya yafuatayo:-

(i) Kuongeza idadi ya dawa, vifaa na vifaa tiba ngazi ya zahanati kutoka aina 254 mwaka 2015 hadi kufikia aina 451 mwaka 2023.

(ii) Kuongeza idadi ya dawa, vifaa na vifaa tiba ngazi ya kituo cha afya kutoka aina 414 mwaka 2015 hadi kufikia aina 828 mwaka 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dawa zilizoongezeka zipo katika miongozo ya Serikali na hivyo zinalipiwa na Bima ya Afya kwa wanufaika wa mfuko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuongeza dawa Serikali imeboresha miundombinu, uwepo wa vifaatiba, huduma za maabara pamoja na rasilimali watu. Hata hivyo, Serikali inatambua kwamba kuna maeneo ya nchi ambayo uboreshaji huu haujafikia, hivyo ipo katika mikakati wa kuyafikia maeneo hayo.