Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?

Supplementary Question 1

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia fursa hii. Je, ni lini Serikali itatupatia minara ya mawasiliano katika Kata ya Tangazo na Kijiji cha Namgogori hakuna kabisa mnara wa mawasiliano ili wananchi wangu waweze kufurahia huduma hii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, maeneo ambayo ameyataja baada ya Bunge lako Tukufu tukutane ili tuweze kuyaweka vizuri na tutume wataalam wetu wakafanye kazi na baada ya hapo tuhakikishe kwamba tunafikisha huduma ya mawailiano, ahsante sana.(Makofi)

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Same Magharibi, Kata za Milimani kuna shida sana ya mitandao. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja kuziangalia Kata hizo za milimani vilevile, ziletewe huduma ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mathayo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Same Mashariki pamoja na Magharibi nilifanya ziara katika maeneo yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja. Ni kweli kuna changamoto lakini habari njema kwa wananchi wa Same ni kwamba, Mheshimiwa Rais ametoa fedha kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasiliano katika Kata zaidi ya 12 katika Wilaya nzima ya Same. Kwa hiyo, naamini kwamba katika maeneo ambayo yatakuwa bado yana changamoto tutatuma wataalam wetu waende wakajiridhishe. Kama tutahitaji kuongeza nguvu ya minara iliyopo tutafanya hivyo, kama tutahitaji kuweka minara mipya basi tutafanya hivyo, lengo likiwa ni kutatua changamoto ya mawasiliano kwa wananchi. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Jimbo langu la Manyoni Mgharibi Halmashauri ya Itigi kuna vijiji vya Mhanga, Tulieni, Mnazi na Vijiji Itagata na Vijiji vya Lulanga havina mawasiliano kabisa. Je, Serikali iko tayari sasa kuingiza katika mpango ujao wa bajeti vijiji hivi navyo vipate huduma ya minara.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira kuu ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inafikisha huduma ya mawasiliano. Kwa sababu ameiomba Serikali kama iko tayari, Serikali tuko tayari kuhakikisha kwamba tunaingiza katika mpango ujao wa kuhakikisha kwamba tunafikisha huduma ya mawasiliano, nakushukuru sana.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?

Supplementary Question 4

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa kila Mbunge anayesimama anaomba minara na maeneo mengi hata Mjini mtandao unasumbua. Ni upi mkakati wa Serikali kutumia satellite ili kuondokana na changamoto hii ya mawasiliano ambayo hata maeneo ya Mijini yenye mabonde na miteremko kumekuwa na vurugu sana za kukosekana kwa mawasiliano. Ni upi mkakati wa Serikali wa kutumia satellite ili mawasiliano yapatikane nchi nzima?(Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mikakati mingi. Serikali iliingia kwenye utatatibu wa Ujenzi wa Mkongo wa Taifa ili tuondokane na matumizi ya microwave ambayo ilikuwa na changamoto kubwa sana, ni ya gharama lakini kulingana na jiografia ya nchi yetu ilivyo ilileta changamoto kubwa. Vilevile, kuna maeneo ambayo tunatumia satellite.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa maelekezo mahsusi ili tuanze mchakato wa kupata satellite yetu kama nchi. Tunaamini kwamba kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetatua chanagamoto nyingi sana za mawasiliano ambayo ni mchango mkubwa sana katika uchumi wa sasa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaji–engage na kila teknolojia inayoibukia ili kuhakikisha kwamba kwanza kabisa tuwe na teknolojia rahisi na inayoweza kwenda kutatua matatizo katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mara nyingine unakuta kuna mnara hapa lakini sehemu ya pili mawasiliano hauwezi ukapata, kunakuwa na dark sports za kutosha. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tumejipanga na tunaendelea na uchambuzi wa kina kuangalia ni teknolojia ipi ambayo itakuja kutupa majibu sahihi kwa ajili ya kutatua changamoto ya mawasiliano kwa wananchi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?

Supplementary Question 5

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naomba na mimi niulize swali. Ni lini mawasiliano yatafika Ilolanguru, Chagu, Songambele, Ubanda na Mumbala? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nashon, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa bado tuna changamoto baadhi ya maeneo katika nchi yetu lakini tunakwenda awamu kwa awamu. Tunapeleka minara 758 vilevile tumefanya tathmini ya vijiji 2116, baada ya hapo tunapeleka minara 600 na baada ya hapo tutapeleka minara 1000. Ninamuomba Mheshimiwa Mbunge aniletee maeneo hayo kwa maandishi ili niyaweke katika mpango wa utekelezaji wa awamu inayokuja, ahsante sana.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, ni lini minara ya simu itajengwa maeneo ya Endahagichang, Tumati Juu, Qalodaginwe, Aidurdagawa, Qamtananat na Migwa?

Supplementary Question 6

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri naomba niweke kumbukumbu sawa ya majina haya. Miqaw, Aidurdagawa, Qamtananat, Endahagichan.

Swali langu la nyongeza, Je, ni lini sasa minara hii unakwenda kuijenga hasa vijiji nilivyotaja na Endahagichan?

Swali la pili, kwa kuwa umefika Jimbo la Mbulu Vijijini na wewe mwenyewe umeona kabisa. Ninaimani hakuna sababu ya kufanya tathmini kwa kuwa umefika mwenyewe na minara haipo katika vijiji nilivyovitaja na iko mbalimbali. Je, ni lini sasa unaweka kwenye mpango huu unaokuja ili vijiji hivi vikapata mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakubaliana na namna ambavyo amesahihisha majina namna anavyoyatamka lakini pia nakubaliana na hali halisi ya changamoto ya mawasiliano katika Jimbo la Mbulu Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifanya ziara na Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake na tulipita meneo mengi. Maeneo mengi yalikuwa na changamoto ya mawasiliano lakini ukubwa wa tatizo tumeupunguza. Mheshimiwa Rais amekubali kutoa fedha kwa ajili ya kupeleka huduma ya mawasiliano katika Kata zifuatazo:-

Kata ya Endahagichan yenyewe ambapo tumepata mtoa huduma wa Airtel pia kuna Kata ya Eshkesh ambayo pia tumepata Artel, kuna Kata ya Geterer ambayo imepata Tigo, kuna Kata ya Masqaroda wamepata TTCL, Kata za Yaeda Ampa na Yaeda Chini wote wamepata Halotel na TTCL. Kwa hiyo, tunaendelea kupunguza ukubwa wa tatizo la changamoto ya mawasiliano ndani ya Jimbo la Mbulu Vijijini. Hivyo tunaamini kwamba awamu ijayo vijiji ambavyo tumesema tutavifanyia tathmini vitakapokamilika tutafikisha huduma ya mawasiliano. Ahsante.