Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kwa miaka mitano iliyopita, Tanzania ilipata kiasi gani kutoka katika Mfuko wa Fedha za Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa (LDCF) ?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali namba moja, kwa kuwa NEMC ndiyo taasisi pekee Tanzania ambayo ina uwezo wa kuomba fedha kupitia huu mfuko wa kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi. Je, Serikali inashirikishaje taasisi nyingine pamoja na NGO katika kuwajengea uwezo ili waweze kuomba fedha na kuzipata kwa haraka?

Swali namba mbili; Je, kwa kuwa Zanzibar fedha hizi pia zinatumika. Je, Serikali haioni haja ya kusaini memorandum of understanding na taasisi moja Zanzibar kama vile ZEMA ili kuweza kuimarisha uratibu na kuwajengea uwezo Wazanzibar ili fedha hizo ziweze kutumika kwa ufanisi zaidi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano Mazingira hasa kupitia Baraza la NEMC tunao utaratibu wa kutoa uelewa kwa wale ambao wanakuja kuandika miradi na kuileta kwetu, zaidi wale ambao watakuja na miradi endapo miradi hiyo itakuwa haijakamilika taarifa zake, hapo ndipo tunawaita na kuwapa uelewa na kuwafahamisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kama kutakuwa na taasisi inataka kuandika miradi na hasa inataka kuleta kwetu basi tupo tayari kwenda kuwapa uelewa ili lengo na madhumuni wawe na ujuzi na utaalam mzuri wa kuandika miradi ambayo itakwenda kusaidia kutatua changamoto za wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Zanzibar tunao ushirikiano na usimamizi mzuri sana wa fedha za miradi na ndiyo maana miradi mingi haijakwama na inaendelea vizuri kwa upande wa Zanzibar na upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendeleza ushirikiano huo ili lengo na madhumuni tutatue changamoto za wananchi hasa za kimazingira na zile ambazo zina lenga katika kubaliana na mabadiliko ya tabianchi. Nakushukuru.

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kwa miaka mitano iliyopita, Tanzania ilipata kiasi gani kutoka katika Mfuko wa Fedha za Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa (LDCF) ?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mradi ambao unatekelezwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini ya Unguja kwa upande wa Zanzibar, mradi huo wa EBA ambao umedhaminiwa kupitia Mfuko huo ambao Mheshimiwa Waziri umetamka mradi wa EBA lakini mradi huo utekelezaji wake ilikuwa ni 2018 mpaka 2022, ukomo wa mradi huo tayari umeshakamilika.

Je, Wizara yako ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba mradi ule ambao tayari uko kule Wilaya ya Kaskazini Unguja kwenye Vijiji vya Matemwe na Shehia ya Mbuyutende unakamilika? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najibu swali la Mheshimiwa Usonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie Watanzania kwamba azma ya Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kwamba inatatua changamoto zote zinazokabili wananchi hasa changamoto zinazokabili kwenye upande wa mabadiliko ya tabianchi. Azma nyingine kubwa ni kuhakikisha kwamba miradi yote iliyokwishaanzishwa kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, ikiwa inasimamiwa na fedha kutoka nje, tutahakikisha kwamba miradi hii inakamilika ili sasa iweze kunufaisha wananchi na wananchi waweze kunufaika na hiyo miradi na mambo mengine yaende. Nakushukuru.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kwa miaka mitano iliyopita, Tanzania ilipata kiasi gani kutoka katika Mfuko wa Fedha za Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa (LDCF) ?

Supplementary Question 3

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mifuko hii ambayo inatenga fedha kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi iko mingi na Mheshimiwa Rais aliposhiriki mkutano kule Scotland aliwasisitiza Mataifa makubwa waheshimu ahadi zao na kutenga hizo fedha. Tatizo na changamoto imekuwepo katika kukosa utaalam.

Je, Wizara iko tayari kuvishirikisha Vyuo Vikuu, Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, SUA na Chuo Kikuu cha Zanzibar katika kupata ule utaalam wa kuandika hayo maandiko ili tupate hizo fedha?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, takribani miradi mingi tumekuwa tunawashirikisha wataalam hasa wataalam kutoka Vyuo Vikuu. Tumekuwa na miradi mingi na miradi hii mara nyingi kwenye masuala ya utafiti tunawashirikisha wanafunzi na walimu wa vyuo vikuu, hata kwenye masuala ya maandiko ya hii miradi kwa maana ya hizo proposal pia huwa tunawapa nafasi ya kuchukua mawazo yao ili lengo na madhumuni tuweze kupata mawazo ya kitaalam kwenye miradi hii, kwa sababu wenzetu wanapokuja kukagua miradi hii huwa zaidi wanaangalia utaalam ambao tumeutumia na zile pocedure ambazo tumezipitia katika kuimarisha miradi hii. Kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuko tayari na kwa sababu tumeshaanza hilo jambo. Nakushukuru.