Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 521 2023-06-05

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, kwa miaka mitano iliyopita, Tanzania ilipata kiasi gani kutoka katika Mfuko wa Fedha za Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa (LDCF) ?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge Wa Donge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hadi sasa imeweza kutekeleza miradi minne ambayo inatekelezwa pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Fedha tulizo pokea ndani ya miaka mitano kutoka Mfuko wa Nchi Zinazoendelea (Least Development Countries Climate Fund-LDCF) ni Kiasi cha Dola za Marekani Milioni 19,343,743.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa za miradi yote minne kwa kina inapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais www.vpo.go.tz.
Aidha, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kutafuta fedha zaidi kutoka kwenye Mfuko wa LDCF ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kadri fursa zinapopatikana kwa pande mbili za Muungano wetu.