Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ni utaratibu gani umewekwa wa kuwapatia mikopo wavuvi wadogo wa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo na kuonesha jinsi gani Serikali ina wajali wavuvi. Maswali yangu mawili ya ziada ni kama ifuatavyo: -

Swali la kwanza; je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu ya mikopo kwa wavuvi wadogo ili iende sambamba na mafunzo ya uvuvi wa kisasa?

Swali langui la pili; je, Serikali imejipangaje kuhakikisha masharti ya mikopo hiyo haiwakwazi na kuwabana wavuvi wadogo? Ahsante.(Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nami pia nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Angelina Adam Malembeka kwa maswali mazuri na ya msingi.

Kwanza nimwondoe shaka kwa sababu haya ni maelekezo ambayo tumepewa na Marais wetu wawili, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Mwinyi kwamba kabla ya mikopo hiyo ni lazima sasa tuwapatie watu elimu ambayo itawasaidia kutumia kwa usahihi mikopo hiyo ambayo itatolewa, kwa hiyo jambo hilo tutalitekeleza kabla mikopo hiyo kuwafikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la masharti, jambo hilo ndio la msingi ambalo sasa hivi tumekuwa tukifanya kwamba tumepunguza masharti kwa kiwango kikubwa na asilimia kubwa ya hii mikopo haina riba, ni mikopo ambayo tunawawezesha tukianza na kuwapatia utaalam wa kisasa, ahsante sana. (Makofi)

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ni utaratibu gani umewekwa wa kuwapatia mikopo wavuvi wadogo wa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wavuvi wadogowadogo hasa Wilaya ya Ukerewe tayari wameshaunda vikundi na taratibu zote za mikopo wameshafata. Je, ni lini Serikali itawapatia mikopo ili waweze kununua nyavu na kuvua kwa halali na kuachana na uvuvi haramu?( Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge Dada yangu Mheshimiwa Furaha Matondo kwamba sehemu ya mikopo ya awamu ya kwanza ambayo tulitoa karibu asilimia 80 ya mikopo ilienda Kanda ya Ziwa kwa maana ya Ziwa Victoria, ni kwa sababu tu waombaji ni wengi na kiwango cha mikopo kilikuwa kidogo. Kwa hiyo sisi tutaendelea kuwazingatia kwa kadri ambavyo tunakuwa tukipokea fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo jambo hilo lipo katika mapango wa Serikali. Ahsante sana.(Makofi)