Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 530 2023-06-05

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, ni utaratibu gani umewekwa wa kuwapatia mikopo wavuvi wadogo wa upande wa Zanzibar?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua mahitaji makubwa ya mikopo kwa wavuvi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinakamilisha maandalizi ya mradi wa uchumi wa buluu (Tanzania Scaling Up Sustainable Fisheries and Acquaculture Management Project – TASFAM) utakaotekelezwa Tanzania Bara na Zanzibar. Mradi huu unafadhiliwa na Benki ya Dunia (World Bank) na utawawezesha wavuvi wa Tanzania Bara na Zanzibar kupata mikopo ya masharti nafuu kupitia taasisi za kifedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, katika juhudi za kusaidia wavuvi wadogo, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Uvuvi Bahari Kuu (DSFA) ina programu za kuwawezesha wavuvi wadogo upande wa Zanzibar kwa kuwapatia mafunzo ya uvuvi wa kisasa pamoja na fursa za upatikanaji wa mikopo ya zana bora za uvuvi kutoka Taasisi mbalimbali za kibenki ikiwemo Benki ya Kilimo Tanzania (TADB).