Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia fedha za ujenzi wa Soko la samaki Bagamoyo?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa mamalishe wengi waliokuwepo katika soko la zamani wamekosa nafasi katika soko jipya. Je, Serikali haioni umuhimu wa kufanya ujenzi wa dharula katika jengo la mamalishe ili kuwanusuru mamalishe waweze kufanya shughuli zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Bagamoyo ina wavuvi wengi ambao wanavua bila kuwa na utaalam. Je, Serikali ina mpango gani wa kutuma watu kuja kutoa mafunzo ya ubora na dhana bora ili wavuvi wasiweze kugombana na Serikali mara nyingi katika uvuvi wao?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo la kwanza ni mpongeze vile vile Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo kwa kufatilia sana jambo hili na bahati nzuri katika soko analolieleza mimi binafsi nimefika na nimejionea hali halisi. Kwa hiyo, sisi kwa kushirikiana na Halmashauri yake tutazungumza na Halmashauri ili tuone namna bora ya kutekeleza huo udharura wa kuwasaidia wale mama lishe ambao walikosa nafasi katika soko la awali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili kuhusu wataalam, nimhakikishie tu kwamba wataalam tunao na tutawatuma ili waweze kupeleka elimu ya utaalam wa uvuvi kwa wananchi wake, ahsante sana.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia fedha za ujenzi wa Soko la samaki Bagamoyo?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga soko la kisasa la samaki katika Kata ya Mbweni ili wananchi waweze kujipatia kipato lakini kuiletea Serikali mapato?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba Mheshimiwa Mbunge ameeleza jambo jema kuhusu soko la kisasa la uvuvi katika Kata ya Mbweni ambalo lipo katika sehemu ya mipango yetu kama Wizara, kikubwa tu sasa hivi ni kwamba tunatafuta fedha na tukishapata fedha katika maeneo yote ya kimkakati tutajenga kama ambavyo tunataka kutekeleza. Ahsante sana.