Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 529 2023-06-05

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamalizia fedha za ujenzi wa Soko la samaki Bagamoyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu : -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo n Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Muharami Shabani Mkenge, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Soko la Samaki Bagamoyo limejengwa kwa fedha za Serikali kupitia Halmashauri ya Bagamoyo na limeshaanza kutumiwa na wadau wa uvuvi. Kwa sasa soko hili lina miundombinu ya jengo la mnada, jengo la kuhifadhia samaki, jengo la maliwato, jengo la kuhifadhia taka, kibanda cha askari/mlinzi na jengo la kukaangia samaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukamilisha soko hili kuendana na michoro iliyopo, inahitajika kuongezewa jengo moja la kukaangia samaki, jengo la mama lishe, jengo la maduka na jengo la ofisi. Aidha, katika mwaka 2024/2025, Serikali imepanga kujenga miundombinu hiyo iliyosalia katika soko hilo kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (Agriculture and Fisheries Development Programme - AFDP).

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, katika mwaka 2023/2024, Serikali kupitia programu ya kuendeleza kilimo na uvuvi itaweka vichanja kumi (10) vya kuanikia dagaa, mahema mawili (2) ya kukaushia samaki kwa kutumia nguvu ya jua na mtambo mmoja wa kuzalisha barafu katika eneo la karibu na soko hilo.