Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwezesha Shule za Kata kuwa pia za Kidato cha Tano na Sita kutokana na kuongezeka kwa ufaulu?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, kuna Halmashauri zenye uwezo wa kuanza mchakato huu kwa kutumia mapato ya ndani kuweza kuweka hii miundombinu. Ni nini commitment ya Serikali kuzisaidia Halmashauri hizi kukamilisha utaratibu huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili je, kama kuna shule zenye miundombinu na ziko tayari kubadilisha baadhi ya madarasa kuwa ya kidato cha tano na sita. Je, Serikali iko tayari kuruhusu watumie hostel za binafsi wakati wanasubiri kujenga mabweni?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimo, kwanza kuhusu Halmashauri ambazo zina uwezo wa kujenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu uko wazi kama, Halmashauri ina uwezo wa kujenga miundombinu inayohitajika kwa ajili ya shule yenye mkondo wa Kidato cha Tano na Sita hawakatazwi kujenga miundombinu hiyo lakini ni lazima wafuate taratibu za kukaguliwa na Mkaguzi wa Elimu kwa kuomba usajili wa Kidato cha Tano na Sita kutoka Wizara ya Elimu na kisha shule hii iweze kupandishwa hadhi. Lakini kama wana uwezo wa kujenga hawakatazwi kuweza kujenga lakini wafuate taratibu za usajili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili kuhusu shule ambazo tayari zina miundombinu. Kama kuna shule ambazo tayari zina miundombinu hii hawakatazwi nao kuandika Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili na tuweze kukagua kuona miundombinu iliyopo na kisha kuwasiliana na Wizara ya Elimu kuweza kuomba sasa usajili wa mkondo wa Kidato cha Tano na Sita. Hivyo, niwaombe wenzetu wa Manispaa ya Moshi Mjini kama wanazo shule ambazo tayari wanaziona zinakidhi vigezo basi waombe kwa maandishi kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na tuweze kutuma timu kwa ajili ukaguzi na kisha kuwasiliana na wenzetu wa Wizara ya Elimu kuweza kuona ni namna gani tunapandisha hadhi shule hizi.