Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 519 2023-06-05

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwezesha Shule za Kata kuwa pia za Kidato cha Tano na Sita kutokana na kuongezeka kwa ufaulu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiongeza shule za Kidato cha Tano na Sita kulingana na uhitaji. Kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023, Serikali ilisajili jumla ya shule 23 ambazo zilikuwa Shule za Kata kuwa Shule za Kidato cha Tano na Sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na jitihada za kuongeza shule za Kidato cha Tano na Sita katika Halmashauri zote nchini kwa kuongeza miundombinu ya mabweni, madarasa mabwalo kwa kuzingatia upatikanaji wa fedha na uhitaji.