Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa Kiwango cha lami barabara ya Getifonga – Mabogini – Kahe?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri yenye matumaini kutoka Serikalini na nina hakika wananchi wangu wa Mabogini na Kahe watakuwa wamepata faraja kubwa sana. Pamoja na hayo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza tunaishukuru Serikali ilitenga shilingi milioni 475 kutengeneza barabara ya TPC, Samanga hadi Chemchem lakini tamanio la wananchi hawa ilikuwa ni kutengeneza daraja kwenye mto Ronga unaounganisha vijiji vya Samanga na Chemchem.

Je, Serikali ina mpango gani kutengeneza daraja hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili barabara ya International School Kibosho KNCU hadi kwa Raphael haijakamilika kwa kiwango cha lami.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara hii? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Profesa Ndakidemi, kwanza ni hii barabara ya Samanga – Chemchem kuhitaji daraja katika mto unakopita.

Kwanza kama alivyosema yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge Serikali ilitenga shilingi milioni 475 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii na tutaangalia katika bajeti tunayoenda kuanza hii ya TARURA ya mwaka 2023/2024, kuona imetengewa kiasi gani kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili na tutamwelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Kilimanjaro kuweza kuelekeza fedha mara moja kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili hili la International School hadi Kibosho barabara hii. Serikali itaendeleza ujenzi wa barabara hii kadri ya upatikanaji wake wa fedha na tutaangalia Mheshimiwa Mbunge katika bajeti hii inayokuja kuona ni namna gani ambavyo tunaweza tukatenga fedha kwa ajili ya kwenda kuanza ukarabati wa kiwango cha lami kwenye barabara hii.