Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 517 2023-06-05

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga kwa Kiwango cha lami barabara ya Getifonga – Mabogini – Kahe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii iko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020 kuijenga kwa kiwango cha lami ambapo hadi sasa TARURA – Mkoa wa Kilimanjaro wamekamilisha usanifu kwa kiwango cha lami na inahitaji shilingi bilioni 28.59 ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 TARURA imetenga shilingi milioni 158.85 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida kwa urefu wa kilomita 12 katika barabara hiyo na kazi imekamilika. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa urefu wa kilometa 1.2.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili barabara hiyo iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.