Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiruhusu wafanyabiashara wazawa wa kusindika kahawa Mkoa wa Kagera kununua kutoka kwa wakulima?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Ishengoma Kikoyo, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa malengo ya Serikali ni kuhamasisha uchumi ambao ni shindani katika ununuzi wa kahawa;

Je, Serikali haioni sasa itoe kibali cha wanunuzi binafsi kushindana na AMCOS kununua kahawa moja kwa moja kutoka kwa wakulima?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa kahawa inaendeshwa kwa Bodi ya Kahawa;

Je, Serikali haioni kwamba ni muda mwafaka kuleta Sheria ya Bodi ya Kahawa hapa Bungeni ikafanyiwa marejeo ili kuendana na uchumi wa sasa? Nakushukuru.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, Serikali imeweka utaratibu ambao unaruhusu pia wawekezaji binafsi kununua kupitia katika AMCOS, ambapo wao wanakusanya. Na ninaomba tu niliweke wazi hapa lieleweke vizuri; AMCOS hanunui kahawa, anachokifanya yeye ni ku-aggregate na baadaye ndipo wanunuzi binafsi wanakwenda kununua kupitia kahawa iliyokusanywa. Kwa hiyo tutakachokifanya ni kuboresha mazingira zaidi ili wakulima wanufaike na bei lakini vilevile na waagizaji binafsi wapate uhakika wa kahawa yao.

Mheshimiwa Spika, la pili, kuhusu marejeo ya sheria; kutokana na kuwa na Agenda Maalum ya 10/30, hivi sasa tunafanya marejeo katika sheria zetu zote ili kuhakikisha kwamba zinaendana na mipango tuliyonayo ya kukuza sekta ya kilimo kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030, ikiwemo sheria ambayo pia inaongoza zao la kahawa.