Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 506 2023-06-02

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO K.n.y. MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isiruhusu wafanyabiashara wazawa wa kusindika kahawa Mkoa wa Kagera kununua kutoka kwa wakulima?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka utaratibu wa uuzaji na ununuzi wa kahawa za wakulima kupitia vyama ya ushirika ili kuondoa uuzaji wa kahawa katika mifumo isiyo rasmi na kuimarisha biashara ya mazao nchini. Aidha, kupitia mfumo huo wafanyabiashara wazawa waliowekeza kwenye viwanda vya kuongeza thamani na kusindika kahawa Mkoani Kagera wanaruhusiwa kununua kahawa kwenye minada ghafi inayoendeshwa na Bodi ya Kahawa. Kupitia utaratibu huo wanunuzi wazawa wanapata nafasi ya kushindana kununua kahawa moja kwa moja kwa wakulima kama ilivyowasilishwa na vyama vyao vya msingi (AMCOS).