Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga skimu katika Bonde la Eyasi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, tarehe 20 Machi, 2023 tulisaini mikataba ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mabonde 22 ya kimkakati hapa nchini Tanzania likiwemo Bonde la Eyasi. Kwa hiyo maana yake skimu zote za Eyasi zitajengwa katika mwaka wa fedha unaokuja.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 2

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu ya Serikali ambayo hayajakidhi swali langu, kwa sababu Skimu za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ambazo nimezitaja, siyo skimu mpya, ni skimu ambazo zimekuwepo na zimekuwa zikifanya kazi. Tatizo miundombinu yake imeharibika na hivyo hazifanyi kazi sasa.

Mheshimiwa Spika, swali; Je, lini mtapeleka fedha kwenye skimu hizi kwa ajili ya ukarabati ili ziweze kufanya kazi inayostahili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wananchi wetu wakulima hawana taaluma juu ya utumiaji wa miundombinu ya umwagiliaji kwa maana ya kwamba hawana taaluma;

Je, ni nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba wanakuwa na maarifa na taaluma ya kutosheleza kutumia miundombinu ya umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika majibu yangu ya msingi nimeeleza vyema kabisa tunayo mabonde 22 ya kimkakati. Katika Mkoa wa Kigoma tunafanyia kazi Bonde la Mto Malagarasi na Bonde la Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Spika, katika maziwa na mito hii miwili ambayo nimeisema ndani yake skimu hizi zinapatikana. Kwa hiyo Serikali imeamua ifanye kazi kubwa kwanza ya upembuzi yakinifu kwenye mabonde haya ambayo pia ndani yake itajumuisha skimu ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitamka. Kwa hiyo nimwondoe hofu kwamba skimu ambazo amezitamka ni ndani ya mkakati wa Serikali katika utekelezaji wa haya mabonde ambapo kazi imekwisha kuanza na ujenzi utaanza mwaka wa fedha ujao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu elimu; tumeajiri wahandisi wa umwagiliaji wa kila wilaya. Hawa watakuwa na jukumu pia la kuhakikisha kwamba wanawapa elimu wakulima wetu juu ya matumizi sahihi ya maji katika kilimocha umwagiliaji. Hivyo wananchi pia wa Jimbo la Buyungu watanufaika na huduma hii kupitia wahandisi wetu walioko wilayani.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 3

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kukamilisha miradi ya umwagiliaji katika Kijiji cha Misyaje na Madaba kilichopo Jimbo la Tunduru Kusini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni mkakati wa Serikali kuhakikisha tunakamilisha skimu zote za umwagiliaji ili wananchi wafanye kilimo cha umwagiliaji. Nitakaa na Mheshimiwa Mbunge kuangalia skimu alizozitaja kama hazipo kwenya mpango wa mwaka wa fedha unaokuja basi tuziingize kwenye mpango ili wananchi waweze kushiriki kwenye kilimo cha umwagialiaji.

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itapeleka pesa kukamilisha mradi wa Lubasazi Kata ya Kolelo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema ninayo orodha ya miradi mingi ambayo tunaitekeleza hivi sasa inawezekana nitashindwa kumpa moja kwa moja mradi wake katika hatua iliyofikia lakini mimi nitakaa naye ili tuangalie katika jedwali letu tuone kama mradi huo haupo basi tuweke katika vipaumbele vyetu.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji katika maeneo ya Mavimba, Lupilo, Minepa, Kivukoni, Namilela katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeainisha maeneo mengi ambayo tunakwenda kuyafanyia kazi katika mwaka wa fedha ujao. Nitakaa na Mheshimiwa Mbunge kuangalia maeneo ambayo ameyataja kama hayajajumuishwa basi tuweze kuyaweka katika mpango wetu ili kuhakikisha wananchi hao pia wanafanya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 6

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi;

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuanzisha miradi ya umwagiliaji kwenye maeneo ya wakulima wadogo wadogo wa chai eneo la Igomini Tarafa ya Igomini Halmashauri ya Njombe?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nataka kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hii ni hoja ambayo Mheshimiwa Mbunge alishaifikisha katika Wizara ya Kilimo na tumemuahidi baada ya Bunge hili la bajeti namwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ndugu yangu Raymond Mndolwa waongozane na Mheshimiwa Mbunge kwenda kufanya tathmini katika maeneo yaliyotajwa ili tuweze kuwasaidia wakulima wa chai katika eneo hilo.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 7

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini skimu ya umwagiliaji ya Mwamapuli itaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika skimu zaidi ya 42 ambazo tutakwenda kuzijenga katika mwaka wa fedha huu ambao unaishia na ambao unaendelea ni pamoja na Skimu ya Mwamapuli. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo liko ndani ya utekelezaji wa Serikali.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Serikali itajenga skimu za umwagilaiji kwa kutumia maji ya Mto Rwiche katika manispaa ya Kigoma Ujiji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwenye mradi wa umwagiliaji kutumia Bonde la Rwiche tunachosubiri hivi sasa ni ile barua ya kutokuwa na kipingamizi ambayo baada ya hapo tutanza utekelezaji mara moja. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zimeshakamilishwa ndani ya Serikali tumebakiza kutoka kwa Mhisani tukipata letter of no objection tunaendelea.