Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 500 2023-06-01

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati Skimu za Umwagiliaji za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji Kakonko?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Skimu za Umwagiliaji Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ni miongoni mwa skimu zilizoko katika Wilaya ya Kakonko zinazounda mabonde 22 ya kimkakati. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kupitia mshauri elekezi katika Skimu za Buyungu, Nyakanyezi, Mgunzu, Kayonza, Muhwazi, Ruhuru na Chulanzo zilizoko katika Wilaya ya Kakonko.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetenga fedha za kuanza ujenzi wa skimu zinazounda mabonde 22 ya kimkakati ambapo Skimu za Katengera, Ruhwiti na Muhwazi ni miongoni mwa skimu hizo.