Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama za matibabu kwa akina mama wanapokwenda Kliniki Sumbawanga?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, ninapenda kujua;

Je, ni kwa nini sasa sera hii haitekelezeki kikamilifu, kwa sababu wanawake wajawazito na watoto chini ya miaka mitano bado wanalipishwa kwenye suala zima la afya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wazee zaidi ya miaka 60 bado pia wanatozwa pesa wanapokwenda kutibiwa;

Je, kwa nini sera hii haitekelezeki?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo anashirikiana na Waheshimiwa Wabunge wa mkoa wake kufuatilia masuala muhimu ya afya katika mkoa wake.

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza, ni kwa nini sera hii haitekelezwi kwa asilimia 100 kama ilivyozungumzika. Ni kama maeneo mengine, wote tunajua kuna kipindi tulipitia kwenye shida ya upungufu wa dawa, kwa hiyo kunapokuwa na upungufu wa dawa na vifaa tiba basi linaathirika eneo hili kama yanavyoathirika maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, lakini pia unakumbuka hapa wakati wa bajeti yetu mlizungumzia suala la mtaji kwa MSD. Sasa maana yake MSD ikishapata mtaji badala ya kutegemea fedha kutoka kwenye vituo, basi sasa ule mnyororo wa upatikanaji wa dawa hautakatika tena kama ambavyo umekuwa ukikatika, na sasa tutaweza kuhakikisha kwamba sasa dawa zitakuwa zinapatikana wakati wote na vifaa tiba vinapatikana wakati wote, na akina mama wanaweza kupata huduma kama ambavyo inatajwa na sera. Tumeshaainisha, Mheshimiwa Waziri ameunda tume imeonesha kwamba tunahitaji bilioni 167 kuweza kuhudumia wananchi katika eneo hili.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu wazee linafanana na hili lingine. Kwanza niseme tu kwamba tumeagiza kila kituo cha afya, kila zahanati, kila hospitali kuwepo na dirisha la wazee. Na tunawaomba wenzetu wakuu wa wilaya na wakurugenzi wasimamie eneo hili la akina mama na eneo la wazee kuhakikisha hili takwa la kisera linatekelezwa ipasavyo, ahsante. (Makofi)