Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 499 2023-06-01

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza gharama za matibabu kwa akina mama wanapokwenda Kliniki Sumbawanga?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sera ya Afya ya mwaka 2007 kifungu Na. 5(3) na (4)(c) kinaelekeza kuwa huduma za afya ya uzazi ikiwemo kuhudhuria kliniki, wakati wa uchungu, wakati wa kujifungua, na baada ya kujifungua pamoja na uzazi wa mpango zitakuwa zikitolewa bila malipo.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa wito kwa watumishi katika vituo vya kutolea huduma za afya kutowatoza gharama za uzazi wanawake wote wanaofika vituoni kupata huduma ya afya ya uzazi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.