Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO K.n.y. MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, kwa nini Serikali imehamisha Kituo Kidogo cha Polisi Tumbe?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa vile Waziri amekiri kwamba kituo hiki kutokana na uchakavu tayari kimeondoka; na tayari kutokana na mahitaji na eneo lile ni kubwa, kuna miradi mikubwa ya Serikali ambayo ipo sasa: -

a) Je, Serikali haioni haja ya kuweka kituo cha dharura katika eneo hili la Tumbe?

b) Je, Wizara iko tayari kwenda kukaa na ofisi ya mkuu wa wilaya pamoja na halmashauri kuangalia eneo kubwa au kupatiwa eneo ambalo litatosha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi, ni kweli kabisa kwamba eneo hili lina matumizi makubwa kwa kuwa pia kuna miradi mikubwa ambayo inahitaji kituo cha polisi. Lakini kituo cha polisi cha dharura kinaweza kikapatikana endapo tu mamlaka za halmashauri husika zitatenga jengo ambalo litakuwa na sifa ya kutumika kama kituo cha polisi.

Mheshimiwa Spika, suala la eneo; kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, ni jukumu la halmashauri sasa kutafuta eneo ambalo tunakwenda kujenga kituo kipya. Na Wizara iko tayari kutoa ushirikiano kwa mamlaka za halmashauri hiyo ili kituo hicho kiweze kujengwa haraka sana.