Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 498 2023-06-01

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO K.n.y. MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali imehamisha Kituo Kidogo cha Polisi Tumbe?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, shughuli na huduma za Kituo cha Polisi Tumbe kilichopo Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba, zimehamishwa toka Tumbe kwenda Kituo cha Polisi Konde. Sababu ya kufanya hivyo ni uchakavu wa jengo lililokuwa linatumika kama kituo cha polisi ambalo ni mali ya Shehia ya Tumbe Mashariki. Jengo hilo halifai tena kwa matumizi ya kazi za polisi. Eneo hilo pia ni finyu na limezingirwa na nyumba za makazi ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kutumia fursa hii kumshauri Mheshimiwa Mbunge kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni kupata eneo kubwa zaidi lenye angalau ukubwa wa square meters 3,000 kwa ajili ya kujenga kituo cha polisi eneo hilo la Tumbe. Wizara kupitia Jeshi la Polisi itaunga mkono katika ujenzi wa kituo hicho kipya, ahsante.