Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Kata ya Bokwa na Songe Kilindi?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nitoe shukrani za dhati sana kwa Serikali yetu kwa kutujengea daraja hili ambalo lilikuwa linaleta usumbufu mkubwa sana kipindi cha mvua. Baada ya shukrani hizo, sasa nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata hizi mbili za Songwe na Bokwa kuna ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami; je, Serikali iko tayari kuweka taa katika eneo hilo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kuna Madaraja mawili ya Chakwale na Nguyami ambayo yanunganisha Wilaya za Kilindi na Gairo. Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa barabara zote zinazojengwa na zinazopita kwenye miji mikubwa ama centers kubwa, maelekezo ni kwamba ni lazima tuweke taa kwa ajili ya matumizi ya usiku katika miji yote ambayo ni mikubwa. Kwa hiyo kwa barabara hiyo ambayo inajengwa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tathmini itafanyika na tutahakikisha kwamba tunaweka taa.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la pili, tumeshakamilisha usanifu wa kina mwaka huu wa fedha kwa Madaraja yote mawili ya Chakwale na Nguyami ambayo yanaunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Tanga, na tumepanga fedha, kwamba mwaka 2023/2024, Madaraja yote hayo mawili ya Chakwale na Nguyami yanakwenda kuanza kujengwa, ahsante. (Makofi)