Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wake wa kurudisha Reli ya Mtwara – Mbamba Bay na eneo la Mchuchuma?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri na ya kuleta tumaini ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza;

a) Je, ni lini sasa mtaanza mchakato wa kuwashirikisha wadau kuhusu ujenzi huo?

b) Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari sasa kuambatana na Mheshimiwa Manyanya na Mheshimiwa Agnes Hokororo, ili kwenda kufanya mikutano kwenye maeneo haya mawili ili wananchi waelewe kabisa kwamba, huo mradi sasa ni kweli utaenda kuanza?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la mchakato wa kwanza katika ujenzi huu wa standard gauge kupitia mfumo huu wa Public Private Partnership kwa njia ya ubia, tayari tumeitisha kikao tarehe 15 ya mwezi wa sita, mwezi huu, ambapo kitashirikisha Wizara yetu ya Ujenzi na Uchukuzi, pamoja na Wizara ya Viwanda, Uwekezaji na Biashara na Wizara ya Madini pamoja na taasisi zake zote pamoja na wadau wote ambao wanashiriki katika uchimbaji wa makaa ya mawe. Na kwa hivyo basi, nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge wa Mikoa hii ya Ruvuma pamoja na Mtwara kushiriki katika mkutano huu pamoja na Lindi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, kuhusu kuambatana kwenda site; niko tayari kuambatana na Waheshimiwa aliowatamka, Mheshimiwa Angelina Manyanya pamoja na Agnes Hokororo na yeye mwenyewe Mheshimiwa Dkt. Ntara, ili tukapate kutoa elimu na kuwaelimisha wananchi katika maeneo hayo kuhusu uwepo na ujio wa mradi huu muhimu katika Mtwara Corridor.

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wake wa kurudisha Reli ya Mtwara – Mbamba Bay na eneo la Mchuchuma?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PALAMAGAMBA J. M. A. KABUDI: Mheshimiwa Spika, nashukiuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Napenda kujua ni lini Serikali itakarabati reli kutoka Kilosa – Mikumi hadi Kidatu, ili ianze kufanya kazi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Palamagamba Kabudi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge amefuatilia jambo hili kwa ukaribu. Tumetenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa reli hii ya Kilosa – Mikumi, na tutaanza rasmi mwezi wa saba mwaka huu kwa ajili ya kuihuisha tena reli hii ianze kufanya kazi kama ilivyokuwa inafanya kazi miaka ya zamani. Ahsante.

Name

Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wake wa kurudisha Reli ya Mtwara – Mbamba Bay na eneo la Mchuchuma?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Watanzania tuna shauku kubwa;

Je, ni lini reli yetu ya kisasa ya mwendokasi itaanza kutoa huduma kwa wananchi kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Reli hii ya mwendokasi (SGR) kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro, kilometa 300 itaanza kutoa huduma mwezi wa saba. Hivi sasa mwezi huu wa sita tunategemea kupokea mabehewa yenye ghorofa na hatimaye mwezi wa saba tutapokea kichwa. Na kwa kuwa tayari miundombinu yote testing na kila kitu kimeshafanyika katika njia hii ipo tayari kwa ajili ya kuanza mara baada ya mabehewa haya yatakayoingia mwezi huu wa sita na vichwa vitakavyoingia mwezi wa saba.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wake wa kurudisha Reli ya Mtwara – Mbamba Bay na eneo la Mchuchuma?

Supplementary Question 4

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mpango wake wa kujenga reli kutoka Tunduma mpaka Bandari ya Kasanga na Kabwe?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, reli hii ya kutoka Tunduma mpaka Rukwa, katika mwaka wa fedha ujao tutaanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa awali, ahsante.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wake wa kurudisha Reli ya Mtwara – Mbamba Bay na eneo la Mchuchuma?

Supplementary Question 5

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante, ninataka kujua, je, ni lini mabehewa 37 yaliyokuwa kwenye karakana ya reli yakikarabatiwa kwa ajili ya safari za Kigoma – Dar es Salaam yataingia kwenye reli na kuanza kazi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng'enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mabehewa aliyoulizia Mheshimiwa Mbunge ni kweli tunakarabati mabehewa 37, na kila mwezi tunakarabati mabehewa 22, 20 za mizigo na mbili za abiria. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wasafiri wote kutoka Kigoma kwamba mwezi ujao mabehewa haya yataanza kufanya kazi. Ahsante. (Makofi)