Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 494 2023-06-01

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, Serikali imefikia wapi katika mpango wake wa kurudisha Reli ya Mtwara – Mbamba Bay na eneo la Mchuchuma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili wa ujenzi wa reli ya Standard Gauge ya Mtwara – Mbamba Bay na matawi yake ya kuelekea Liganga na Mchuchuma. Aidha, taarifa hiyo ya upembuzi yakinifu na usanifu ilipendekeza kuwa mradi huu utekelezwe kwa utaratibu wa ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Public Private Partnership – PPP).

Mheshimiwa Spika, ni matarajio yetu kuwa marekebisho ya Sheria ya PPP yatakayofanyika hivi karibuni yatasaidia kuwapata wawekezaji kwa ajili ya kujenga reli hii muhimu. Naomba kuchukua fursa hii kumuomba Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Mtwara na Ruvuma kuwa na subira wakati Serikali inashughulikia kwani suala hili litapewa kipaumbele na Serikali katika mwaka 2023/2024 ili kukamilisha taratibu za kumpata mjenzi, ahsante.