Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; je, ni lini Serikali itafungua kituo cha afya cha Kata ya Lyamugungwe na kupeleka vifaa tiba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata kama kuna fedha imetengwa, na kama bado haikutengwa basi tutatenga kwenye mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 2

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Tarafa ya kimkakati ya Mbuji yenye kata tano?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni kipaumbele cha Serikali kuhakikisha inajenga vituo hivi vya afya katika kata za kimkakati. Na tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata tuweze kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya hiki.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Tarafa ya Nangaru na Milola?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni kipaumbele cha Serikali kuhakikisha inajenga vituo vya afya kwenye kata na tarafa za kimkakati kote nchini. Na tutatafuta fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024 na kama hakuna fedha hizo basi tutatengea bajeti kwenye mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi, je, ni lini Serikali itajenga wodi za wanaume na wanawake katika Kituo cha Afya cha Ifingo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata ili ifingo waweze kupata fedha hii. Lakini vilevile nichukue nafasi hii kuomba Wakurugenzi wa halmashuri kuwa wanatenga fedha kwa ajili ya ujenzi na umaliziaji wa zahanati na vituo vya afya kwenye halmashauri zao. Serikali Kuu imeshapeleka fedha nyingi sana kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya hivi na zahanati hizi na fedha nyingi ya vifaa tiba na wao wasaidie sasa.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 5

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata ya Igundu na Namura katika Jimbo la Mwibara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itajenga vituo hivi vya afya kadiri ya upatikanaji wa fedha na tutaangalia tena katika mwaka wa fedha unaofuata ili tuweze kuweka kipaumbele fedha hiyo iweze Kwenda. Na kama haipo tutatengea kwenye mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 6

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

a) Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Udekwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili linatoka katika Mkoa wa Simiyu, Wilaya ya Maswa, Wilaya ya Binza;

b) Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Binza? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili haya ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata hii ya Budekwa ipo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo. Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wake kadiri ya upatikanaji wa fedha; na tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata kama kuna fedha imetengwa, ili iweze kwenda mara moja kujenga.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la kituo cha afya hiki alichokiulizia kilichoko Mkoani Simiyu, tutaangalia vilevile kuona ni namna gani kama fedha imetengwa basi iweze kwenda mara moja kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki cha afya.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, napenda kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo: -

Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata ya Vudee na Siji?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya Mundee na Suji kadiri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 8

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba kwenye vituo vya afya viwili vilivyokamilika; Kituo cha Afya cha Magazini na Ligela?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata kama kuna fedha imetengwa basi tutahakikisha iweze kwenda mara moja na kama haipo basi tutatenga katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 9

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kumalizia Kituo cha Afya Samunge, Kata ya Samunge?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata ili tuweze kutenga fedha hii ya kumalizia Kituo cha Afya cha Samunge.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 10

MHE. JEREMIAH A. MRIMI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Iramba kilichochakaa sana?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata na kuipa kipaumbele kata hii na kuweza kupeleka fedha kadiri ya ilivyotengwa.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 11

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, ningependa kuuliza kuna vituo vya afya vingi nchini ambavyo havijamaliziwa OPD. Ni lini OPD zitamaliziwa katika vitu vya afya ambavyo havina OPD?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa awamu katika halmashauri mbalimbali hapa nchini kwa ajili ya umaliziaji wa majengo haya. Tunaendelea kutafuta fedha kuona ni namna gani tunapeleka kwa ajili ya umaliziaji wa majengo ambayo bado hayajakamilika. Na kwa yale yaliyokamilika Serikali inaendelea pia kupeleka vifaa tiba ili huduma kwa wananchi iweze kuanza kutolewa kwa wakati.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Supplementary Question 12

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya Lupila kwa sababu, majengo yake yamechakaa sana na ni ya muda mrefu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Kituo cha Afya Lupila kimetengewa fedha za World Bank na kitaenda kujengwa katika mwaka huo wa fedha. Vilevile kuna maombi maalum ya Mheshimiwa Mbunge ya Kituo cha Afya Mfumbi ambayo nayo yanafanyiwa kazi, ili kituo cha afya hicho kiweze kujengwa.