Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 493 2023-06-01

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya Ihanu – Mufindi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga shilingi bilioni moja ambapo shilingi milioni 500 ni kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mgololo, shilingi milioni 150 ni kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha upasuaji kwenye Kituo cha Afya Mbalamaziwa na shilingi milioni 350 ujenzi wa Kituo cha Afya Mdabulo. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 halmashauri kupitia mapato ya ndani imetenga shilingi milioni 562 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la OPD Kituo cha Afya Ihalimba na shilingi milioni 120 ukamilishaji wa jengo la OPD Kituo cha Afya Mapanda.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Afya kwenye kata za kimkakati kote nchini kikiwemo Kituo cha Afya Ihanu.