Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, Serikali haioni kutoa fedha za ujenzi wa vituo vya afya kwa kigezo cha idadi ya tarafa ni kuwanyima wananchi vituo vya afya?

Supplementary Question 1

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Wilaya ya Nyamagana ina tarafa moja tu, na idadi ya wananchi ni kubwa. Ukigawa kulingana na tarafa mbalimbali maana yake unawanyima fursa wananchi wa Nyamagana kupata huduma stahiki hasa walio pembezoni kule Ngwanyima na Kishiri;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuangalia, hasa idadi ya wananchi na umbali wa kupata huduma kwenye maeneo hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa hali ileile ya Nyamagana inalingana kabisa na hali ya Jimbo la Magu, hasa Kata ya Mwamanga na Kata ya Lutale;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuziona kata hizi ambazo ziko mbali na huduma katika vituo vya afya kwenye wilaya zao? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mabula; la kwanza kuhusu Jimbo la Nyamagana kuwa na tarafa moja tu.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali iliangalia maeneo ambayo ni pembezoni na yako mbali na huduma za afya kabisa na kuyapa kipaumbe na kuwa ni kata za kimkakati. Hili la Nyamagana tunalipokea kama Serikali na kuweza kuangalia ni namna gani tutapeleka timu ya kufanya tathmini na kuona vituo vya afya vya Serikali vilivyopo katika jimbo hili na kuona uwezekano wa kutenga bajeti ya kuwaongezea vituo vya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la kata hizi alizozitaja ikiwemo Kata ya Mwamanga katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kata hizi za kimkakati kote nchini, ikiwemo katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Tutaangalia katika bajeti ya mwaka 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu, ili tuweze kuanza na ujenzi wa kata hizi za Mwamanga na nyingine ambayo aliitaja Mheshimiwa Kiswaga.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, Serikali haioni kutoa fedha za ujenzi wa vituo vya afya kwa kigezo cha idadi ya tarafa ni kuwanyima wananchi vituo vya afya?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona: -

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Makambako inahudumia Halmashauri mbili, yaani Jimbo la Lupembeā€¦

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa? Nenda moja kwa moja kwenye swali, unataka Serikali ikujibu nini?

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nimekuelewa. Nataka Serikali, katika Jimbo la Makambako tarafa moja ina majimbo mawili, kila tarafa iwe na jimbo lake ili Serikali inapopanga mipango ya kuhudumia tarafa tuweze kuhudumiwa vizuri kwenye Tarafa yetu ya Makambako. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tunalipokea hilo na tutaangalia katika bajeti zilizotengwa tuone tupeleke kituo cha afya.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, Serikali haioni kutoa fedha za ujenzi wa vituo vya afya kwa kigezo cha idadi ya tarafa ni kuwanyima wananchi vituo vya afya?

Supplementary Question 3

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, Jimbo la Singida Mashariki, Kata ya Misupaa pamoja na Isuna hazina vituo vya afya;

Je, ni lini Serikali itajenga vituo hivyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutajenga vituo vya afya hivi katika Kata ya Isuna na nyinginezo kule Singida kadiri ya upatikanaji wa fedha, na tutaangalia kwenye bajeti inayofuata kuona ni kiasi gani kimetengwa ili Serikali ianze ujenzi huo.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, Serikali haioni kutoa fedha za ujenzi wa vituo vya afya kwa kigezo cha idadi ya tarafa ni kuwanyima wananchi vituo vya afya?

Supplementary Question 4

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Katika Tarafa ya Kipatimu Kata ya Chumo tumekamilisha ujenzi wa kituo cha afya mwezi uliopita.

SPIKA: Unataka Serikali ifanye nini?

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali italeta vifaa tiba, dawa pamoja na watumishi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga shilingi bilioni 7.1 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba kwenye vituo vya afya mbalimbali hapa nchini, na tutaangalia katika bajeti hii ambayo imetengwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba hivi; kama Tarafa ya Kipatimu kwenye kituo cha afya alichokitaja Mheshimiwa Ndulane imetengwa na tutapeleka vifaa tiba huko.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA K.n.y. MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, Serikali haioni kutoa fedha za ujenzi wa vituo vya afya kwa kigezo cha idadi ya tarafa ni kuwanyima wananchi vituo vya afya?

Supplementary Question 5

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, kile Kituo cha Afya cha Bweri ni kituo cha muda mrefu, lakini kimeshindwa kwisha na kwa hiyo, wananchi wa eneo lile wanashindwa kupata huduma;

Je, ni lini Serikali itamalizia hicho kituo ili wananchi wapate huduma nzuri za kituo cha afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata kama kuna fedha imetengwa kwa ajili ya umaliziaji wa Kituo hiki cha Afya cha Bweri ili tuweze kumalizia, na kama haijatengwa tutaangalia katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.