Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, lini vifaatiba vya Hospitali ya Wilaya ya Buchosa vitanunuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii kuishukuru sana Serikali kwa kutekeleza jambo hili ambalo kwa muda mrefu nimekuwa nikilipigia kelele, kwamba fedha milioni 500 wakati vifaa havikuwa vimenunuliwa. Sasa ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ina mahitaji ya watumishi 166 lakini waliopo ni watumishi 39 pekee na hili linafanya vifaa hivi vishindwe kutumika ipasavyo;

Je, Serikali iko tayari kufanya commitment ya lini watumishi hawa watapelekwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kumbukumbu za wananchi wa Buchosa hasa katika Kisiwa cha Kome kwenye Kituo cha Afya cha Nyamisri waliwahi kuahidiwa kupelekewa X–Ray mpya, wakati ule Waziri wa TAMISEMI akiwa dada yangu, Mheshimiwa Ummy Mwalimu;

Je, Serikali inaikumbuka ahadi hii au imekwishakuisahau; na kama inaikumbuka, iko tayari kuitimiza? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la kwanza la nyongeza la Mheshimiwa Shigongo la kuhusu ni lini Serikali itapeleka watumishi katika Hospitali ya Wilaya ya Buchosa: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imetangaza ajira za sekta ya afya 8,070 nchini, na hii ni kwenda kujazia maeneo yenye upungufu wa watumushi, ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa. Hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika hawa watakaoajiriwa hivi karibuni nao watapata watumishi hawa katika hospitali ya wilaya.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la X-Ray iliyoahidiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, katika Kituo cha Afya Nyamisi; tutatekeleza ahadi hii kadiri ya upatikanaji wa fedha. na tutaangalia katika bajeti ya mwaka 2023/2024 kama kituo hiki kimetengewa fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba basi x-ray iwe kipaumbele kupelekwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi.