Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 491 2023-06-01

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -

Je, lini vifaatiba vya Hospitali ya Wilaya ya Buchosa vitanunuliwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eric James Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 ilipeleka Bohari Kuu ya Dawa fedha shilingi bilioni 34 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba kwa hospitali za halmashauri 67 zilizoanza ujenzi mwaka wa fedha 2019/2020 ikiwemo Hospitali ya Wilaya ya Buchosa ambapo kila hospitali ilitengewa shilingi milioni 500.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023 Hospitali ya Wilaya ya Buchosa imepokea fedha za ruzuku kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba shilingi milioni 800 pamoja na vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 596.

Mheshimiwa Spika, taratibu za kusimika vifaatiba vilivyopokelewa unaendelea kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Buchosa. X–Ray mashine tayari imefungwa tangu mwezi Aprili 2023. Tunsubiri wataalamu wa mionzi kutoka Tume ya Nguvu za Atomic Tanzania kukagua na kutoa kibali ili utoaji wa huduma uweze kuanza.