Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa, mnada huo hakuna choo, hakuna maji na wananchi wanapeleka mifugo yao mara kwa mara pale na mnakusanya fedha nyingi pale. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuchukua hatua ya dharura kujenga choo na kupeleka maji pale ikisubiria mpango mkubwa?

Swali la pili, je, kwa kuwa mnada huo pia Wizara ndiyo inakusanya fedha, kwa nini fedha hizo ambazo mnazikusanya isitumike kwa ajili ya kukarabati mnada huo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, jambo la kwanza tukiri changamoto ambazo Mheshimiwa Mbunge amezieleza na akiwa anahitaji hatua za dharura. Nimuondoe shaka kwamba hizo hatua za dharura kwa mahitaji hayo kama ya vyoo pamoja na maji basi tutawaelekeza wataalamu katika maeneo hayo waweze kuyafanyia kazi haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, pili kuhusu makusanyo ya fedha ambazo zinakusanywa pale kwamba ndiyo zifanye ukarabati, nimwambie tu kwamba mnada ule unahitaji ukarabati mkubwa na ndiyo maana tunataka tufanye tathmini na tuujenge kwa viwango ambavyo vinastahili. Kwa hiyo tutalietekeleza hili kama ambavyo Serikali imepanga katika mipango yake, ahsante. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Nimekuwa nikiuliza mara kadhaa kuhusu ujenzi wa Soko la Samaki katika Jimbo langu la Mchinga, Kata ya Mchinga lakini mara zote nimekuwa nikipewa tu ahadi, ahadi, ahadi! Sasa naiomba Serikali inipe commitment kuhusu suala la ujenzi wa hilo soko la Samaki, ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza ninakiri kwamba Serikali ni kweli imekuwa ikitoa ahadi kwa ajili ya ujenzi wa soko la samaki katika Jimbo la Mchinga na jambo hilo mpaka sasa hivi bado halijafanyika, sababu za kutofanyika ni kwamba mpaka sasa Serikali tunatafuta fedha ili tufanye usanifu wa kina na baadae tulijenge soko hilo. Kwa hiyo, commitment ya Serikali iko pale pale kwamba soko hilo tutalijenga na wakati uliopo sasa ni kutafuta fedha, ninaamini kabla hatujamaliza hii miaka yetu miwili kuna hatua ambayo tutakuwa tumeifanya na kufikia. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Supplementary Question 3

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii.

Kwa kuwa, Waziri wa Mifugo alishatembelea mnada wa Duka Bovu katika Wilaya ya Monduli na akaahidi ukarabati utaanza mara moja; je, ukarabati huu utaanza lini? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mnada katika eneo la Monduli ambalo Mheshimiwa Mbunge ameutaja upo katika mipango ya Serikali, tunachosubiri tu ni malipo ambayo tukiyapata kutoka Hazina basi sehemu ya fedha hizo zitakwenda kwa ajili ya ukarabati. Ahsante sana.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Supplementary Question 4

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini mtaboresha miundombinu kwa minada ya Kibaya, Dosidosi na Sunya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu awali, kwa sasa tunatafuta fedha ili tuhakikishe kwamba hiyo minada ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja tunaikarabati na kuitengeneza kwa viwango ambavyo vinavyotakiwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge waondoe shaka wananchi kwamba Serikali ya Awamu ya Sita itatekeleza kama ilivyoahidi. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Supplementary Question 5

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Mnada wa Kata ya Soya ni kati ya minada mikubwa ambayo inafanya shughuli za uuzaji wa mifugo kwa maana ya mbuzi, ng’ombe, kondoo pamoja na punda lakini mnada ule miundombinu yake ni chakavu.

Je, Serikali mko tayari kuutembelea mnada ule nakujionea halia halisi ili muweze kutenga fedha itakayoweza kukarabati mradi huo ili wakulima wa mifugo waweze kuutumia mnada ule kwa tija na kwa maana ya afya kwa watumiaji? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tuko tayari kufika katika eneo la Soya, bahati nzuri ni karibu hapa tunaweza tukapanga tu baada ya muda wa Bunge tukafika na kujionea hali halisi ili tuweze kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati huo, ahsante sana. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Supplementary Question 6

MHE. IDD K. IDD: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwa kuwa Halmashauri ya Msalala imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ajili ya ujenzi wa uzio wa mnada wa Kata ya Burige, sasa ni lini Serikali italeta fedha kukamilisha ujenzi wa miundombinu katika mnada huo wa Burige?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwanza tuipongeze Halmashauri ya Msalala kwa kutenga fedha kwa ajili ya uzio wa mnada ambao Mheshimiwa Mbunge ameuainisha. Serikali tulishaweka commitment yetu kwa ajili ya kumalizia mnada huo, commitment yetu iko pale pale isipokuwa kwa sasa hivi tunaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha mnada huo. Ahsante sana. (Makofi)