Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 490 2023-05-31

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza

Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa mnada wa ng'ombe na mbuzi wa Olokii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara ya mifugo hapa nchini kwa kujenga na kukarabati minada ya mifugo ya awali, minada ya upili na minada ya mipakani. Kwa sasa kuna jumla ya minada 504 ya awali, 17 ya upili na 12 ya mpakani. Mnada wa Olokii (Themi) ni moja ya minada ya upili ambao upo chini ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 na Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali imejenga na kukarabati minada 12 katika maeneo mbalimbali nchini. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itafanya usanifu wa miundombinu ya mnada wa Olokii (Themi) ili uweze kuingizwa katika Mpango wa Bajeti wa mwaka wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati.